skills za kitaa

Friday, September 14, 2012

WANAFUNZI 23 WA SHULE YA MSINGI KAPUNGA WANUSURIKA KIFO BAADA YA KUOKOTA MIKATE INAYOSADIKIWA KUWA NA SUMU.



The President extends his warmest wishes to all those celebrating the Jewish HIgh Holidays.


Ni katika shamba la Kapunga Rice Project.

Wazazi wacharuka na kuanza kujenga shule mpya mahali alipobomoa mwekezaji.
Zaidi ya shilingi milioni 2.5 zachangwa papo hapo.

Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.

Wanafunzi 23 wa Shule ya Msingi Kapunga,Kijiji cha Mapogolo,Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya wamenusurika kifo baada ya kula mikate inayosadikiwa kuwa na sumu mnamo mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bwana Ramadhani Nyoni na mzazi mmoja wapo wa watoto waliokumbwa na janga hilo la kusikitisha na kuhatarisha uhai.

Mzazi huyo ambaye hakupenda jina lake kutaja amesema yeye ilimlazimu kununua lita 20 za maziwa,kisha kuwanywesha watoto hao na kuokoa maisha yao ambapo hali zao zimetajwa kuendelea vema.

Wakazi wa kijiji hicho wakionekana kukerwa na kitendo hicho iliwalazimu kuitisha mkutano wa hadhara na kuazimia kujenga shule mpya ili kuwaondoa watoto katika shule iliyopo katika shamba la mwekezaji.

Mbali ya wananchi kukerwa na vitendo vya kikatili vya mwekezaji huyo,pia Walimu wamefurahia uamuzi wa wanakijiji kuamua kujenga shule mpya katika himaya ya kijiji ili kuondoa adha ya kutembea umbali wa kilometa 52 kwenda na kurudi kutoka Chimala,ambako ndipo walipopanga kutokana na uhaba wa nyumba kijijini hapo na zilizopo shambani kwa mwekezaji walimu hao hufukuzwa mara kwa mara.

No comments: