skills za kitaa

Wednesday, September 12, 2012

Uchaguzi wa urais Somalia umepokewa kama hatua ya kihistoria ya kuelekea kwenye demokrasia


Raia wa Somalia na viongozi wa kisiasa walipokea kwa furaha matokeo ya uchaguzi wa Rais jijini Mogadishu Jumatatu (tarehe 10 Septemba) ambayo yalileta ushindi wa mwanataaluma na mwanaharakati wa jamii ya kiraia Hassan Sheikh Mohamud, kiongozi wa chama cha Amani na Maendeleo.

Katika hotuba yake ya kwanza kwa taifa , Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud alisema, "Sasa ni wakati wa mabadiliko nchini Somalia." [Mahmoud Mohamed/Sabahi]

Mohamud alimshinda aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho Sheikh Sharif Sheikh Ahmed katika duru ya pili ya uchaguzi, 190 kwa 79.

Wachambuzi wameelezea uchaguzi huu kuwa, wa kwanza wa aina yake nchini Somalia kwa zaidi ya miongo miwili, kama ukamilishaji wa historia kwa Somalia na mwanzo wa mpito wa nchi wa kuelekea kwenye demokrasia.

Mchambuzi wa masuala ya kisiasa na profesa wa chuo kikuu Ahmed Moalim Ahmed alisema ushindi wa Mohamud ni mwanzo wa hatua mpya katika mpito wa kisiasa wa Somalia.

"Tunatarajia kuwa hatua hii ya kihistoria ya kuchagua rais mpya kwa nchi itaonyesha kipindi kipya cha utulivu na mwisho wa vita vya wenyewe kwa wenyewe,"," Ahmed aliiambia Sabahi. "Ushindi wa Hassan Sheikh Mohamud kama rais ni ishara kuwa Somalia imeingia kwenye hatua mpya na kipindi cha wababe wa vita kimekwisha."

"Tunatarajia kuwa hali katika nchi itaboreka na kuwa kama Wasomalia tutaweza kuondoa matatizo yoyote ambayo tumeyapitia kwa miaka iliyopita," alisema.

No comments: