skills za kitaa

Wednesday, September 12, 2012

Balozi wa Marekani nchini Libya auawa


Mashambulizi dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Benghazi, Libya.Balozi wa Marekani nchini Libya na wafanyakazi wengine wa ubalozi huo wameuawa kutokana na mashambulizi ya roketi katika mji wa Benghazi yanayohusishwa na maandamano ya Waislamu kupinga filamu inayomkashifu Mtume wao.

Afisa mmoja wa serikali ya Libya amethibitisha kwamba Balozi Chriss Stevens na wafanyakazi wengine watatu wa ubalozi huo waliuawa kwa roketi lililorushwa kwenye gari ya ubalozi. Hata hivyo, haikubainika mara moja kama balozi huyo alikuwamo kwenye gari iliyoshambuliwa, au alikufa usiku wa kuamkia leo, baada ya waandamanaji wenye silaha kuuvamia ubalozi huo mjini Benghazi.

Waandamanaji hao walikuwa wamekasirishwa na filamu moja ya Hollywood ambayo inayakashifu kiongozi wa Waislamu, Mtume Muhammad. Maandamano kama hayo pia yalifanyika mjini Cairo, Misri, ambako maelfu ya waandamanaji waliuvamia ubalozi wa Marekani, lakini bila kuwapo visa vya mashambulizi. 

Wakristo wa madhehebu ya Koptik nao wamekusudia kufanya maandamano kupinga filamu hiyo, wakisema kuwa ni matusi kwa imani za watu wote.

Romney apata mwanya

Mgombea wa urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican, Mitt Romney, amelitumia tukio hilo kuushambulia utawala wa Rais Obama kwa kuwa pamoja na waandamanaji wa Kiislamu wenye siasa kali na sio pamoja na Wamarekani.

No comments: