skills za kitaa

Monday, December 9, 2013

TASWIRA:MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE AKIFUNGA RASMI MKUTANO WA MAWAZIRI WA NCHI ZA MASHARIKI NA KUSINI MWA AFRIKA KUHUSU ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA VIJANA


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa pamoja na viongozi waandamizi waliohudhuria mkutano wa High Level Group hukom Cape Town wakisimama kwa dakika moja kwa ajili ya kumkumbuka hayati Rais Nelson Mandela. Kutoka kushoto ni Bwana Enver Surty, Waziri wa Elimu ya Msingi wa Afrika Kusini, Dr. Festus Mogae, Rais Mstaafu wa Botswana, Mama Salma, Bwana Luiz Loures, Naibu Mkurugenzi Mtendaji, UNAIDS, Dr. Julitha Onabanjo, Naibu Mkurugenzi Mkuu, UNFPA, Bwana Qian Tang, Naibu Mkurugenzi Mkuu-Elimu- UNESCO, Bwana Geeta Rao Gupta, Naibu Mkurugenzi Mtendaji, UNICEF.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akihutubia mkutano wa Mawaziri kutoka nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika kuhusu elimu ya afya ya uzazi kwa vijana wa nchi hizo. Mkutano huo wa siku mbili unafanyika nchini Afrika Kusini katika Mji wa Cape Town tarehe 6-7.12.2013.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wakisikiliza hotuba ya ufungaji iliyokuwa ikitolewa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete huko Cape Town nchini Afrika Kusini tarehe 7.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Rais Mstaafu wa Botswana na Mjumbe wa High Level Group Dr. Festus Mogae wakati wa kikao cha Mawaziri wa Elimu na Afya kutoka nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika unaofanyika Cape Town nchini Afrika Kusini tarehe 7.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipiga picha na Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Bwana Michel Sidibe wakionyesha umuhimu wa dhana nzima ya mkutano wa High Level Group ( YOUNG PEOPLE TODAY, TIME TO ACT NOW) kuhusiana na masuala ya elimu ya afya ya uzazi kwa vjijana katika nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Mawaziri wa Elimu na Afya kutoka nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika wakiapa kwa niaba ya nchi zao kutekeleza majukumu waliyopitisha kwenye kikao cha High Level Group, kuhusiana na elimu ya afya ya uzazi ( comprehensive sexuality education and sexual and reproductive health services) mwishoni mwa kikao cha siku mbili kilichofanyika huko Cape Town.Picha na John Lukuwi

No comments: