skills za kitaa

Thursday, January 9, 2014

Soma Justin Bieber na Selena Gomez mapenzi tele, wajiachia na baba yake Bieber


Inaonekana mambo yanazidi kurudi kwenye mstari kati ya mastaa wawili Justin Bieber na Selena Gomez ambao kwa muda mrefu mapenzi yao yamekuwa na drama ambazo zilionekana kuupasua moyo wa Selena Gomez, na kutangaza mara kadhaa kuwekana kando.
Siku kadhaa baada ya kuzagaa ripoti kuwa mastaa hao wamerudiana, wameonekana wakitoka pamoja na kwenda mapumzikoni Jumamosi, January 4.
Mfanyakazi wa SeasCape Beach Resort katika eneo la Santa Cruz, aliiambia KSBW kuwa Bieber na Selena Gomez waliambatana na baba yake Justin Bieber, Jeremy Jack na kwamba walilala katika eneo hilo na kuondoka kesho yake asubuhi.
“We were so very excited. He came Saturday night and left Sunday afternoon. He and his friend (were) riding his Segway through the campground and toward Manresa (State) Beach. It was the best thing ever.” Alisema mfanyakazi mmoja.
Hata hivyo, Bieber na Selena hawakutaka kufahamika kwa hiyo walivyaa mavazi tofauti huku Selena akivaa wig kichwani ili iwe vigumu kufahamika.
Lakini mashuhuda waliiambia KSWB kuwa walipogundua kuwa watu wameanza kuwafahamu, walikimbia ili wakajifiche lakini wakiwa katika harakati za kukimbia wig la selena lilianguka na nywele zake ndefu nyeusi zilionekana.

No comments: