skills za kitaa

Thursday, January 16, 2014

Kanye West alimpiga ngumi zaidi ya 30 kijana mdogo aliyewatukana huku Kim Kardashian akishuhudia


Ingawa Kanye West alisema mwaka jana mwishoni kuwa mwaka huu 2014 hatasema maneno mabaya kwa mtu yeyote, ameuanza kwa vitendo vibaya baada ya kumporomoshea ngumi zaidi ya 30 kijana mdogo aliyemtukana mama mtoto wake Kim Kardashian.
Shuhuda wa tukio hilo aliiambia TMZ kuwa kijana huyo aliyesemekana kumtukana Kim Kardashian kwa maneno ya kibaguzi akimuita Kanye kuwa ni n***er (a n***er lover) alijikuta akila kichapo kama anapigwa na mwanamasumbwi baada ya kuketi kwenye kiti kwa dakika kadhaa huku akidhani yameisha.
Shuhuda huyo amesimulia kuwa dakika chache baada ya kumrushia maneno Kim Kardashian na kuelekea kwenye ofisi moja ambapo alikaa kwenye kiti, Kim Kardashian na Kanye West waliingia kwenye ofisi hiyo huku Kanye West akiwa amekasirika, na bila kusema chochote alianza kumpiga ngumi akiulenga uso wake huku mrembo wake Kim Kardashian akishuhudia.
Imeelezwa kuwa kijana huyo alijitahidi kuuzuia uso wake kwa kuukinga na mikono lakini hali ilikuwa tete kwa mvua za ngumi toka kwa Yeezy.
TMZ imeripoti kuwa mtu wa mapokezi alipiga kelele kwa nguvu akimtaka Kanye amuache mtoto huyo ‘stop, stop’ lakini aliendelea. Wahudumu wengine waliingilia kati na kumsukuma Kanye West ili asiendelee kumpiga kijana huyo.
 Baada ya tukio hilo Kanye West alitoka nje ya jengo hilo kivyake na Kim Kardashian akaelekea kwenye ofisi nyingine kwa ajili ya kikao.
Kwa mujibu wa USA Today, Polisi wametoa tamko wakithibitisha kuwa walipokea simu kuhusu tukio hilo na kwamba kijana huyo na watu wengine walimtaja mtuhumiwa kwa jina la ‘Kanye West’, na kwamba maafisa wa polisi wanaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo.

No comments: