skills za kitaa

Tuesday, July 23, 2013

Kate Middleton hatimaye kajifungua mwanawe


Subira yavuta kheri na kheri imevutika nchini Uingereza.
 Mkewe Prince William, Kate Middleton hatimaye kajifungua mwanawe wa kwanza wa kiume ambaye pia atakuwa mtoto wao wa kwanza . Kate alikimbizwa hospitali mjini London kwa gari akiwa ameambatana na mumewe.(Photo dailymail.com)
baby
Little prince - or princess? Royal supporters have both balloons with them as they wait outside the hospital ahead of the birth  Britain rejoices: Monarchists clamour for a better view as the news is revealed outside the Queen's home
Shangwe vifijo na hoi hoi zimetanda katika jiji la Uingereza na vitongoji vyake baada ya mke wa mwana mfalme Kate kujifungua mtoto wa kiume leo Jumatatu 22-07-2013 saa 10.24 jioni .Mtoto wa kifalme huyo anaingia katika kizazi cha nne cha kifalme.
Kate, aliyejulikana awali kama Catherine Duchess wa Cambridge, amejifungua mtoto huyo wa kiume katika hospitali ya St.Mary huko jijini London. Mtoto huyo atakuwa wa tatu katika mstari wa kupata ufalme kutoka kwa babu yake, mwana mfalme Charles, na Baba yake William.
“Mimi na mke wangu tunafuraha kubwa sana kwa ujio wa kuzaliwa mjukuu wetu wa kwanza” alisema Charles kwenye tamko lilotolewa na msemaji wa familia ya kifalme.
“ Maisha ya kuwa babu na bibi wa mjukuu ni ya kipekee sana katika maisha ya mtu. Na leo nina furaha sana kuwa babu kwa mara ya kwanza na tunasubiria kwa hamu kubwa sana kumwona mtoto aliyezaliwa” Alisistiza Charles kwenye tamko hilo.
The waiting crowds cheer as the Queen's Press Secretary Ailsa Anderson with Badar Azim a footman place on an easel in the Forecourt of Buckingham Palace a notification, to announce the birth of a baby boy
Shangwe na hoi hoi zimesikika nje ya eneo la Lindo Wing ambapo ipo hospitali ya St. Mary baada ya tamko hilo kutolewa. Watu wazidi kumiminika kuelekea katika kasri ya kifalme kupate habari zaidi juu ya ujio wa mtoto wa kiume aliyezaliwa.
CHANZO Sunday shomari na www.dailymail.com

No comments: