skills za kitaa

Tuesday, October 16, 2012

Upatikanaji wa huduma ya intaneti waongezeka nchini Somalia


Ingawa bado yako chini kulinganisha na nchi nyengine duniani, matumizi ya intaneti nchini Somalia yanakuja juu kidogo kidogo huku kampuni zikipigania wateja na raia zaidi wakiwa na fursa ya kutumia intaneti katika nyumba zao na sehemu za biashara.
Vijana wa Kisomali wakitumia mtandao wa intaneti katika Mkahawa wa Amudi mjini Mogadishu. [Mahmoud Mohamed/Sabahi]
Idadi kubwa kampuni za simu nchini Somalia - kubwa zaidi zikiwemo Global Internet, Golis Telecom, Telesom na Somtel - wanashindana kutoa huduma za intaneti kwa wateja na mikahawa nchi nzima kupitia mitandao mbali mbali ya minara, satalaiti, na mikonga ya mawasiliano.
"Mwaka wa 2000 watumiaji wa intaneti walikuwa chini ya asilimia 1 (ya raia wote), lakini idadi imepanda juu kwa miaka ya hivi karibuni hadi kufikia kiasi ya asilimia 2 katika mwaka wa 2011, kwa mujibu wa makisio yasiyo rasmi," alisema Abdisalam Mohamed, mkurugenzi wa masoko wa Global Internet, moja ya watoaji wakubwa wa huduma za intaneti katika eneo la kati na kusini mwa Somalia.
Mohamed alisema kampuni mjini Mogadishu sasa zinatoa aina mbalimbali za huduma za intaneti kwa watumiaji binafsi, kama vile DSL, huduma ya intaneti isiyotumia waya na za satalaiti.
Licha ya upatikanaji wake, huduma za majumbani hazijawafikia Wasomali wengi kutokana na ughali wake. "Gharama (za huduma) hizi ni kati ya dola 30 hadi dola 600 kwa mwezi, kulingana na kiwango cha huduma na kasi ya kuunganishwa inayotumiwa na mtumiaji," alisema Mohamed.

No comments: