skills za kitaa

Sunday, July 13, 2014

Dre alala mikia wizi Feki wa kazi za Beats By Dre


jjWaliokuwa wamiliki wa Beats Eletronics Dr. Dre na mfanya biashara mwenzake Jimmy Iovine wamefungua kesi ya madai dhidi ya mitandao na makampuni ya China yaliyouza bidha feki kwa kutumia jina la bidha ya Beats Eletronics ya Beats By Dre.  Dr Dre akishirikiana na Apple wametoa taarifa kuwa mpaka sasa bidha hizo feki zimetengeneza kiasi cha dola za Marekani bilioni 135.
Dr. Dre ambaye ameuza haki za bidha ya Beats headphones kwa Apple anafanya bidii zote kuzuia bidha feki za China kuharibu bidha zake za Beats By Dre. Tmz imeripoti kuwa kesi ya Dr Dre kwa mtandao huo ambao haujatajwa ni kuzuia na kudai fidia walizo ingiza kupitia kuuza bidha zenye logo ya Beats By Dre ambazo hazina kiwango cha bidha halisi na hivyo kupotosha wateja na kuharibu jina la bidha yake.
Dr Dre akishinda kesi hii ya madai basi fidia atakayolipwa itamfanya awe billionaire.

No comments: