skills za kitaa

Sunday, July 6, 2014

BAADA YA KUWA MAJERUI NEYMAR AWATAKIA KILA LA HERI WENZAKE AKISAFIRISHWA KWENDA MAPUMZIKONI



Neymar amesafirishwa kwa helikopta kupelekwa Sao Paulo kuanza mapumziko
NYOTA wa Brazil, Neymar anaamini timu yake itashinda Kombe la Dunia bila ya kuwa na yeye.
Mchezaji huyo wa Barcelona aliaga mashineano hayo juzi usiku baada ya kuchezewa rafu na mchezaji wa Colombia, Juan Zuniga.
Mchezaji huyo ameelezea maumivu yake baada ya pigo hilo linalomuondoa Kombe la Dunia mapema akiiacha timu yake imetinga Nusu Fainali na zaidi amewatakia heri wachezaji wenzake wabakize kombe hilo nyumbani.
Neymar amesafirishwa kwa helikopta baada ya tiba ya awali na kupelekwa Sao Paulo kuanza mapumziko. Tayari FIFA imesema inalifanyia uchunguzi tukio hilo kabla ya kumchukulia hatua Zuniga.
Safe journey: Neymar with the president of the Brazilian Football Condederation Jose Maria Marin
Neymar akipewa pole na Rais wa Shirikisho la Soka Brazil, Jose Maria Marin.

No comments: