skills za kitaa

Saturday, August 8, 2015

MWASHIUYA KESHO KUCHEZA NYUMBANI KWAO



Kesho Jumapili, Yanga itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Kimondo FC ya Mbeya, timu hiyo imepania kuonyesha soka safi kuthibitisha ubora mbele ya winga wao wa zamani, Geoffrey Mwashiuya aliyejiunga na Wanajangwani.

Yanga inatarajiwa kuondoka jijini Dar es Salaam, leo Jumamosi tayari kwa mchezo huo utakaochezwa kwenye Uwanja wa CCM Vwawa, Mbozi jijini Mbeya ikiwa ni sehemu ya maandalizi yake kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.
Mchezo huo ni sehemu ya makubaliano ya kimkataba ya uhamisho wa Mwashiuya aliyejiunga Yanga na kugeuka lulu kutokana na uwezo wake kuwavutia wengi.
Ofisa Habari wa Kimondo, Chriss Kashililika amesema timu yao ina jeuri ya kuifunga Yanga kwa kuwa ina kikosi imara kwani ina wachezaji wanaofanana kiuchezaji na Mwashiuya zaidi ya nane.
“Maandalizi ya mchezo yapo vizuri kwa sababu timu ipo kambini, Yanga ni timu kubwa na tunaiheshimu lakini kwa jinsi tulivyojipanga kwa mchezo huo uhakika na ushindi ni mkubwa.
“Kama Yanga walidhani wametukomoa kwa Mwashiuya basi wanajidanganya, tuna kina Mwashiuya kama nane, kwa hiyo pengo lake limezibika na tutafanya vizuri,” alijigamba Kashililika. 

na Saleh Ally

No comments: