skills za kitaa

Sunday, June 23, 2013

KANYE WEST NA KIM KARDASHIAN MTOTO WAo ANAITWA NORTH WEST




Rapper Kanye West na Kim Kardashian wamekuwa wasiri kuhusu mtoto wao kuanzia jinsia yake kabla hajazaliwa lakini hata baada ya kuzaliwa wamekuwa na kigugumizi cha kuliweka wazi jina la mtoto wao wa kike waliyempata June 15 mwaka huu.

Japokuwa wameficha jina la mtoto wao, cheti cha kuzaliwa cha mtoto huyo kimeongea…chanzo cha kuaminika kimeuambia mtandao wa TMZ kuwa cheti hicho kimeonesha jina la kichanga wao kuwa ni ‘North West’.

Well, wameamua kutumia dira zaidi kupata jina la mtoto au labda ni kwa sababu baba nae anajina la dira ‘West’ ambalo linatoka kwenye familia yake,marehemu mama yake aliitwa Donda West.Tetesi za awali ziliwahi kulitaja jina hili, lakini baadae ikasemekana wanaweza kutumia utaratibu wa familia ya Kardashians ambayo majina yao lazima yaanze na herufi ‘K’.

Kwa mujibu wa US Weekly, mtoto huyo tayari ameshapata jina la ki-digital yaani a.k.a na anaitwa ‘Nori’ kama ufupisho wa jina lake. Kwa upande mwingine, imesemekana kuwa Kanye West hayuko tayari kufanya biashara kwa kuuza picha za mtoto wake kama alivyowahi kufanya Angelina Jolie na Brad Pitt mwaka 2008 walipouza picha za mtoto wao kwa kiasi cha dola million 14.
Lakini baba North West hapendi kupigwapigwa picha na labda asiingependa mwanae pia aingie kwenye lens za paparazzi, chanzo kimeoja kimesema inawezekana Kim Kardashian akaamua kuzitoa bure picha za mtoto wao kwa kuwa ana hulka ya kupiga picha.
Inasemekana Weezy (36) mwenye mzuka wa ajabu wa kuandika na kutema mistari anaweza kuachia nyimbo nne maalum kwa mwanae Nori..kama alivyofanya swaiba wake Jay-Z alipoachia Glory kwa ajili ya Blue Ivy.

No comments: