skills za kitaa

Saturday, February 7, 2015

Mbasha akana kukitambua kichanga cha mkewe


Emmanuel Mbasha amekiambia kituo cha redio cha SunRise kuwa hajuo kuwa mkewe amejifungua mtoto
Emmanuel Mbasha amekiambia kipindi cha redio cha SunRise -Times FC kuwa hajuo kuwa mkewe Flora Mbasha amejifungua mtoto
Familia ya Mbasha inaendelea kutengeteza vichwa vya habari, baaada ya mchungaji maarufu nchini Gwajima kukanusha kuwa si baba wa mtoto wa Flora Mbasha, mume wa muimbaji huyo wa injili Emmanuel naye ameibuka na kudai kuwa hatambui chochote kuhusu kuzaliwa kwa mtoto huyo.
Mbasha ambaye pia ni muimbaji wa muziki huo wa injili amesema anachojua ana mtoto mmoja wa kike anaeitwa Lizy mwenye umri wa miaka kumi na hizo taarifa za Flora kajifungua anazisikia kwa watu wengine.
Mtoto aliyezaliwa na mwanamuzki wa injili Flora Mbasha
Mtoto aliyezaliwa na mwanamuzki wa injili Flora Mbasha
“Nina mtoto mmoja, nina mtoto mmoja anaitwa Lizy ana umri wa kama miaka 10 hivi! Wewe ndo unanieleza mimi kama amejifungua, kama amejifungua, ni jambo jema na la kumshukuru Mungu,” alieleza Emmanuel Mbasha
Mbasha alikiambia kipindi cha SunRice Times Fc.

No comments: