skills za kitaa

Thursday, June 12, 2014

Mkali wa Hip Hop 50 cent kutoa albam mwaka huu na G-Unit



Kundi la G-unit baada ya kuungana katika tamasha la Summer Jam na kisha kuachia nyimbo mbili ,kiongozi wa kundi hilo 50 cent amejibu swali ambao mashabiki wengi wa HipHop walikuwa wanajiuliza kama kuna uwezekano wakafanya albam ya pamoja.
50 cent akifanya mahojiano na  FOX 29 katika kipindi cha Good Day amesema albam ipo njiani inakuja mashabiki wakae tayari ,
 "Yes…yes utaona albam mwishoni mwa mwezi november " amesema 50
albam hiyo itakuwa ya tatu kwa G-Unit ya kwanza walitoa mwaka 2003 ( Beg For Mercy )2007 T.O.S. (Terminate on Sight).

No comments: