skills za kitaa

Tuesday, September 2, 2014

Kuvuja kwa za Mastaa kwa chunguzwa na Shirika la upelelezi la Marekani (FBI)


Shirika la upelelezi la Marekani (FBI) linachunguza tuhuma kwamba picha za siri za watu maarufu ziliibiwa na kutumwa mtandaoni.
Muigizaji Jennifer Lawrence alikuwa mmoja wa waathiriwa baada ya mdukuzi kutuma picha zaidi ya 60 mtandaoni.
Muigizaji Jennifer Lawrence alikuwa mmoja wa waathiriwa baada ya mdukuzi kutuma picha zaidi ya 60 mtandaoni.
Mastaa hao wapatao 20, akiwemo muigizaji wa kike wa Marekani Jennifer Lawrence, naye picha zake zilivujishwa kwenye mtandao wa Internet.
Inafahamika kuwa baadhi ya picha  hizo zilipatikana katika huduma ya Apple iCloud ambayo husaidi ujumbe uliopo mtandaoni.
Huduma ya Apple iCloud ndio iliyomsaidia mdukuzi asiyejulikana kuchukua picha chafu za Jennifer Lawrence na mastaa wengine 100 na kuzivujisha mtandaoni.
Huduma ya Apple iCloud ndio iliyomsaidia mdukuzi asiyejulikana kuchukua picha chafu za Jennifer Lawrence na mastaa wengine 100 na kuzivujisha mtandaoni.
Apple nao imesema inachunguza kuwa kama akaunti ya iCloud ilifanyiwa udukuzi.
Bi Lawrence, ambaye ni nyota katika filamu za The Hunger Games, ameomba kufanywa uchunguzi baada ya mdukuzi kupata picha, zenye ujumbe wa picha, kutoka simu za mkononi za mastaa kadhaa.
Msemaji wa FBI aliiambia Associated Press kwamba “wako makini na tuhuma hizo na wanalishughulikia suala hilo”.
Naye msemaji wa Apple Nat Kerris alinukuliwa na Reuters akisema kwenye barua pepe; “Huwa tunalinda faragha za watumiaji kwa umakini mkubwa na tunachunguza ripoti hii.”

No comments: