skills za kitaa

Sunday, November 24, 2013

Msome 'Mbabe Chrispini' hapo chini

 MSANII maarufu nchini Lady Jay Dee anatarajia
kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa filamu ya
'The Return of Kidnappe' kwenye ukumbi wa Much More
ndani ya ukumbi wa Club Billicanas.

Kwa mujibu wa  Chrispiani Kirspini 'Mbabe Chrispini'
ambauye ndiye mwandaaji wa ujio huo alisema kuwa
nyota wengine katika  tasnia ya filamu wanatarajia kuwa
waalikwa katika uzinduzi huo.

"Fiamu hii imeelekeza mipango mingi tu katika mazingira
ya watu kijamii,"alisema Chrispin.

Alisema   tayari baadhi ya wadhamini wamejitokeza
kuzamini uzinduzi huo  ambapo Mkurugenzi wa Kampuni
ya TIOT ,Merey Balhabou amejitokeza pamoja
na Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ambapo
wadhamini wengine ni Kamal Steels LTD zote za
Dar es Salaam.


Aidha alisema kuwa uwepowa msanii Lady Jay Dee
ni hali ya unachochea pia uzinduzi huo ni moja ya  kujenga
heshima katika siku hiyo ya November 29 mwaka huu ,
kwani mwana dada huyo ni moja ya wasanii wakubwa barani
Afrika.

Alisema nyota wenye walio alikwa  katika  tasnia hiyo ni
Vicent Kigosi 'Ray' Jacob Stephen 'JB' pamoja na badhi ya  nyota
wengine pia wa tasnia ya muziki kama kama Fareed Kubanda
'Fid Q'.


Chrispiani ambaye ni mhusika kuu wa filamu hiyo  amewataja wasanii wengine waliohusika kuuvaa uhusika ndani ya ujio huo kuwa ni Chuch Hans , Ben Blanko , Eddson Elamu pamoja na  Mwalindu .

No comments: