skills za kitaa

Thursday, February 21, 2013

Chokoraa

MWANAMUZI wa bendi ya muziki wa dansi nchini Khalid Chokoraa amesema akiwa ni
moja wa viongozi wa bendi ya Mapacha Watatu  ameibuka na kumkoromea kiongozio wa bendi mpya
ya muziki huo Mwinjuma Muumin anayeongoza bendiya  Victoria Sound.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Chokoraa amemkoromea Muumin kwa kusema kuwa nyota huyo
amefilisika kimuziki. 



"kitendo chake cha kuujibu wimbo wa 'Shamba la Twanga'
ni ushahidi kuwa enzi zake zimekwisha,"alisema Chokoraa.

Aliendelea kufunguka Chokoraa kwa kutamba kuwa  bendi ya  Twanga kupitia kwa uongozi wa Asha Baraka imwachie yeye kazi ya kumjibu Muumin.

Nyota huyo alienda mbali zaidi na kusema  "hakika kitu alichokifanya Muumin bendi
ya Twanga iniachie mimi kumjibu kwanza mimi na yeye tunatoka sehemu moja Bagamoyo hivyo
awezi kunishinda ."


Tayari bendi ya  'Mapacha Watatu'kwa sasa inajiandaa kwa ajili ya uzinduzi wa albamu mpya itakayozinduliwa mach 2 mwaka huu kwenye ukumbi wa Business Park maeneo ya Victoria jijini Dar es Salaa.

No comments: